Sunday, May 11, 2008

Utangulizi

Masalkheri vijana wenzangu wote popote mlipo ulimwenguni.Karibuni katika maskani yetu tuweze kujadili kwa pamoja mambo yanayotusibu katika maisha ya kila siku na kuyatafutia suluhu.Ninaamini kwamba kwa pamoja tunaweza kwani what man did man can do, yaani alichoweza kufanya mtu hata mwingine nae anaweza.
Uwezo tunao,ila tunacho kosa bado hatujaweka nia au azma ya kuleta mabadiliko katika maisha yetu.Amka kijana mwenzangu,anza kuchukua hatua za kubadilisha maisha yako na wanaokuzunguka leo.Linalowezekana leo lisingoje kesho,kumbuka udongo uwahi ungali maji.
Raslimali ya mwanaadamu ni uzima wake,ukichezea ujana kumbuka fainali uzeeni.Mwili ukishazeeka na kukosa nguvu usitarajie kuja kuweza kufanya jambo uzeeni.Ukiufuja na kuuchezea mwili wako sasa,usijelia mgongo utakapokua haunyooki na viungo vimechoka kwa uzee.Kaa ufikiri kabla hujafikiriwa.Juta kabla hujajutiwa na lia kabla hujaliliwa.

No comments: